Monday, September 16, 2013

AMBER ROSE AJIWEKA MATATANI NA MCHORO WA MSALABA

HALI iliyoibua sintofahamu kutoka kwa baadhi ya mashabiki wake ni baada ya mwanamitindo wa kimataifa nchini Marekani Amber Rose kuonenaka akiwa na tatto ya msalaba kwenye paji la uso wake. Wiki iliyopita Amber alionekana kwenye picha iliyowashangaza wengi baada ya kuchora alama hiyo ya msalaba unaonekana ukiwa umechorwa tofauti hali ambayo baadhi ya mashabiki wamehusisha na imani za kishetani. Msalaba huo ambao umeonekana kutolingana na kutofautiana na misalaba mingine, umeonekana juu ni chini na chini ni juu hali iliyozidi kuleta tafrani. Amber ambaye ni mke wa Rapper Wiz Khalifa ambapo hivi karibuni walifanikiwa kupata mtoto.

No comments:

Post a Comment

Reliable & Affordable Hosting+Web Services